Monday, June 29, 2009

BURIANI PROF HAROUB OTHMAN!

Kweli Duniani tunapita!

Taifa limepoteza msomi, mwanadiplomasia na mwanaharakati wa haki za binadamu ambaye siku zote aliwatetea wanyonge wa Taifa hili, Africa na Duniani kote.

Tutakukumbuka daima Prof Othman, nakuweka kundi moja na kina Prof Chachage kwa kuacha fikra zitakazoishi kwa muda mrefu ndani ya jamii yetu.

Kwaheri Prof Othman.

Saturday, April 4, 2009

SIJUI NIJARIBU UBUNGE?


Wapo wanaosema ndogo, wapo wanaosema zinatosha, wapo wanaosema ziko juu sana. Hata wao wenyewe wanatofautiana mfano ni 'ishu' hiyo hapo juu kama ilivyoelezwa na mbunge wa Karatu Dr. Slaa.
Mi nasema ni nyingi mno ukizingatia mishahara ya watu wetu bado iko chini sana, fikiria pale wahutimu wa vyuo vikuu wanaolipwa mshahara wa laki tatu na nusu. Kwa mbunge anayepata 6,900,000/= kwa mwezi kipato chake ni sawa karibu mara ishirini ya kipato anachopata mhitimu wa chuo kikuu.
Kwa maelezo yoyote yale,hii si sawa!

Thursday, March 26, 2009

TUTAANZAJE UPYA BILA FIKRA MPYA?

Mijadala ni mwanzo wa kuibuka kwa fikra mpya na changamoto kuelekea maendeleo ya kijamii. Pasipo mijadala mawazo yamefungwa, yanabaki vichwani tu. Mijadala isiyokamilishwa na matendo ya kuyatekeleza ni mijadala iliyokufa.Haitufai.

Ni dhahiri yako mengi yasiyo sawa, ndani ya jamii na yanayotuzunguka, ndani ya daladala, radioni kunasikika hotel ya Paradise imeungua, iko Bagamoyo.Bagamoyo gari ya zimamoto hakuna, jamaa anaongea kwa sauti kuuuubwa, anauliza “gari moja ya zima moto shilingi ngapi hata kuishinda wilaya kama Bagamoyo kulimiliki”? Hotel imeungua. Imeteketea. Hatuoni. Hatusikii. Hatubadiliki.

Hapa ndipo watu wanajiuliza,” ni nani aliyeturoga?”, tuangalie kwa uchache baadhi ya mambo.

Elimu yetu, ni kwa vipi inatusaidia kutatua matatizo yetu?, ni kwa vipi inaikabili hali ya umaskini inayotuzunguka?, ni kwa vipi imejipanga kukabilianana mahitaji halisi ya jamii yetu?, ni kwa vipi inapunguza pengo la kiteknolojia lililopo kati yetu na mataifa yaliyoendelea litufanyalo tuendelee kuwaabudu ‘wazungu’ kuwa wenye akili sana kana kwamba waafrika tumezaliwa tukiwa ni “vilaza”?, Inawaandaaje watu wetu kuwa wavumbuzi siku zijazo?, Inawaandaaje watu wetu kulima kilimo cha kisasa?, Inawaandaje watu wetu kujikinga na maradhi kama malaria na kipindupindu?,
Ni kwa vipi imejipanga kukabiliana na mahitaji halisi ya jamii yetu?, tunaambiwa waalimu tulionao ni wachache, nini kinafanyika kuondoa tatizo hili?, na kama kuna linalofanyika ni kwa ubora gani?. Kuna wakati ilikuwa fahari kusoma shule za Serikali kuanzia shule ya msingi hadi sekondari.Hali si hivyo sasa. Aanyebisha na ajitokeze!. Watu wenye uwezo wa kifedha hawapeleki wana wao kwenye shule hizo.Viongozi wetu hawapeleki wana wao shule hizo. Zimekuwa shule za kina Kayumba!, Wenye uwezo wanasomesha wana wao shule za seminary, shule za mtakatifu fulani na fulani, wakilamaliza wanawapeleka vyuo vya nje.Wanatudanganya kwa kuonyesha uzalendo wao kwenye kuchangia mabati ya shule na madawati. Mbona watoto wao hawasomi huko?, Kwa nini tusiwaambie wabunge na madiwani wetu kuwa kama watoto wenu hawasomi shule zetu na nyinyi si wenzetu?, kama watoto wao wangesoma shule zetu, zingekosa walimu?, zingekosa madawati?, wasingezijali?
Turudi kwa walimu, nani asiyejua kuwa huu ni uchaguzi wa mwisho wa wanafunzi wetu wanapokosa vyuo vingine vyooote!, hii imepelekea wanafunzi wanaopata daraja la nne ndio hufikiria kuomba kudahiriwa kwenye vyuo vya ualimu.Bado tunadhani tuna elimu bora?
Mbali na hapo waalimu hao wachache na baadhi wenye ubora mdogo wanahama taaluma yao muda mfupi baada ya kukabiliana na ugumu wa mazingira ya kazi wakiwa ndani ya ajira zao

Uchumi wetu, madini tuliyonayo kwa uchache tukitaja dhahabu, almasi na tanzanite bado hayajatuletea tija ya kutosha. Mwalimu Nyerere aliwahi kutuasa kuwa tuyaache madini yetu hadi pale tutakapoweza kuyachimba wenyewe kwa kutumia wataalamu wetu. Wajanja wakaja na pipi wakatuzidi akili tukawaachia, eti wawekezaji.Wizi mtupu!.Tunaambiwa wanatuachia 3% tu ya mapato, na sisi ndio wenye mali. Si wizi huo?. Geita,Tulawaka, Bulyankulu, Buzwagi, Kahama, North Mara iko siku tutashuhudia mashimo mareeeeeeeefu, sijui tutawajibu nini wana wa wanetu pale watakapotuuliza kilichotoka kwenye mashimo hayo tulikiuza wapi, shilingi ngapi na tulitumiaje kilichopatikana?. Bila shaka uwekezaji ( niuite wizi) huu uliofanyika katika madini yetu mithili ya huo duniani haupo!.Tunaambiwa mmmoja wa mikataba hiyo ulisainiwa Uingereza na waziri husika.Inasemekana shughuli hiyo ilifanyika hotelini. Nani aliyeturoga watized sie?

Samaki, ndio tumeibiwa mpaka basi. Majuzi kuna meli imekamatwa na tani 200 za samaki, kilo moja ni dola 20, tani 200 ni kilo 200,000, hivyo gharama ya wizi ule uliozuiwa ni 4000,000$, kwa kiwango cha kubadilisha dola cha sasa 1300/=, tungepoteza billioni 5.2 fedha za kitanzania. Wajinga ndo waliwao, duh!, wale wachina, wavietinam,ufilipini, indonesia na wakenya watatu, arobaini yao ilikuwa imefika, kesi iko mahakamani sasa. Kazi kwao.Kabla ya hizo arobaini zao, anzia moja, mbili, tatu,……… hadi arobaini, ni shilingi ngapi zilizoibiwa?, kama ndio ilikuwa kamchezo kao jamaa, tuwapigie hesabu 40-1=39; 39 zidisha kwa bilioni 5.2 ni sawa na bilioni 202.8/=.Wizi mtupu!. Tones na tones za samaki wetu wa baharini na maziwani zinaenda Ulaya.Uwiano wa mapato na kinachochukuliwa ( kinachoibwa) ni mdogo saana!. Maziwa na bahari zetu nazo ni shamba la bibi?, kila mtu anavuna na kula!, bibi hana noma!,eti wacha wajukuu wale!, tuseme nini basi kama si kulogwa ni nini?. Nani wa kutukomboa na giza hili?.Hakika bado tungali gizani hata katika mwanga huu!
Wako wapi wenye taaluma ya viumbe hawa wa majini?, Je tuna mabaharia wa kutosha katika shughuli hizi za majini?, Ulinzi wa majini uko bora kwa kiwango kinachostahili?, walikovua samaki wetu hao wezi, je sisi tuna meli gani tunazozitumia kuvua huko?,Au kuvua hatuvui samaki wetu lakini kuibiwa hatutaki?

Maadili yetu, hapa napo panazingua!. Sielewi ni nani mlinzi wa maadili yetu kama si sisi wanajamii wenyewe?, nani anayekemea mmong’onyoko wa maadili unakwenda kwa spidi ya swala katika jamii yetu?, Waangalie dada zetu, ni uchizi kama si uwendawazimu, hakuna nguo za siri tena kwani leo hii ni kawaida kuwaona mabinti wamevaa chupi zikiwa juu ya suruali zao za kubana, wanazionyesha za nini?, wanamuonyesha nani?,ili iweje?. Nguo fupi na viblauzi vya kuishia juu ya kitovu, eti fashion.Sijui. Ila nionavyo tuendako hakuna maelezo ya kutosha kuelezea yatakayojiri kwa wana na wana wa wana wa taifa hili! Mashuleni na vyuoni ndipo yalipotamalaki mambo hayo wanayoita ‘kwenda na wakati’!

Naungana na wanaosema tunahitaji mijadala ya kitaifa katika kutatua matatizo yanayotuzunguka.

Tufanye hivyo!.

Tuanze sasa!

Mijadala hujenga fikra!

Mungu ibariki Tanzania!

Wednesday, March 25, 2009

BILLY GRAHAM AND US PRESIDENTS!

David Frost ndiye muandishi, ni habari inayoeleza nyuma miaka 30 Mazungumzo yao na Billy Graham katika kitabu kiitwacho “Personal thoughts of a public man”

Billy Graham ni mhubiri wa kimataifa, anafahamu siasa za Marekani na amekuwa rafiki wa karibu wa karibu kila raisi wa taifa hilo kubwa kama vile,Harry Truman, Eisenhower, Lyndon Johnson ,John Kennedy, Richard Nixon na Bill Clinton.

Ukurasa wa 95
President Bill Clinton, May 6, 1996 alinukuliwa akisema:

‘I hardly ever go to a place, as Presiident, that Billy Graham has not been there before me preaching. And I feel like a poor substitute, because a lot of the time what I’m trying to do is to get people to lay down the hatred of the heart and reach down into their spirit and treat people who are different from themselves with the same respect that all God’s children are entitled to…………………..
I thank Billy and Ruth Graham for the ministry of their lives’

Ukurasa wa 97;

David Frost, mwandishi wa kitabu hichio: anasema ‘No preacher in the history of this country has had so much access to many presidents as Billy Graham’.



Hapana shaka kuwa alikuwa mshauri wa kisiasa wa wakuu hawa wa Marekani, ushauri uliobeba ukweli na sera zenye kubeba haki na demokrasia.

Marekani ya leo inayoongozwa na Rais Obama, mweusi, ni dhahiri kuwa ni mwendelezo wa harakati fulani za hadharani kama za kina Martin Luther na kina Billy Graham.`

Hapa tunajifunza kuwa viongozi waongozao roho zetu wana nafasi kubwa ku ‘influence’ siasa zetu, hapa Afrika na hasa Tanzania katika kujenga jamii bora zaidi,yenye hofu ya Mungu na kusimamia haki. Na si kuendekeza ufisadi unaolimaliza bara la Afrika. Mfano mzuri wa mapambano haya na harakati za kuipigania haki ni Askofu Desmon Tutu wa Afrika ya kusini. Ambaye wakati Mandela akiwa gerezania alionekana hadharani akiongoza maandamano ya kuidai haki ya usawa ndani ya nchi yao na kuna wakati aliwakemea watawala wa Afrika a kusini, wabaguzi,, kwa sauti kuuuubwa “ Release our leaders”, “Release our leaders”, “Release our leaders”. Bado watanzania tumo katika kifungo cha umasikini, maradhi, ujinga, ufisadi. Nani wapigao kelele mithili ya Desmond Tutu akiwataka watawala wetu na wakoloni wetu wa kale kutuacha huru.


Wako wapi kina Billy Graham wetu Tanzania!

Friday, January 23, 2009

RWANDA ARRESTS REBEL LEADER




Gen Nkunda has said he protects Congo's Tutsis from Rwandan Hutus
Gen Laurent Nkunda, leader of the strongest rebel group in eastern Democratic Republic of Congo, has been arrested in Rwanda.
He crossed the border after resisting a joint Rwandan-Congolese operation to arrest him, both countries say.
Correspondents say it is a startling about-turn by Rwanda, which had been accused of backing Gen Nkunda.
The BBC's Thomas Fessy says there is a sense of relief among residents in Goma who feel the war is nearing an end.
Some 250,000 people fled their homes in the region when Gen Nkunda led an offensive on the city towards the end of last year.
Some 4,000 Rwandan troops entered DR Congo this week to help fight rebel forces in the area.

See detailed map of the area Correspondents say Gen Nkunda's arrest removes one obstacle to peace but other rebel groups remain active.
The UN refugee agency warns that further military action against other rebel groups in the area could lead to a humanitarian disaster.
BBC Africa analyst Martin Plaut says Gen Nkunda has been caught in the rapidly changing diplomatic situation in Central Africa.
LAURENT NKUNDA
Age: 40
Congolese Tutsi
Fought for Tutsi rebels in Rwanda and DR Congo
Accused of war crimes in DR Congo
Studied psychology
Owns a cheese farm
Gen Nkunda had been Rwanda's ally in eastern DR Congo - a Tutsi, like Rwanda's leaders, he guarded their western flank against attacks from the Hutu forces who fled there after the Rwandan genocide of 1994.
But in mid-November Rwanda shifted its position, announcing it would work with the Congolese to destroy the Hutu rebels.
Gen Nkunda did not back the new alliance and so became an impediment to Rwandan plans in the region, causing Rwanda to turn on him, our correspondent says.
The decision earlier this month by a group of Gen Nkunda's top commanders to break away and join forces with government troops gave them their opportunity, he adds.
Henry Boshoff, an analyst from South Africa's Institute for Security Studies, told the BBC that following intense diplomatic pressure in recent months, Rwanda was obliged to arrest Gen Nkunda.
The next step is for the joint Congolese-Rwandan force to tackle the FDLR Hutu rebels, some of whose leaders are accused of involvement in the 1994 slaughter in Rwanda of some 800,000 Tutsis and moderate Hutus.
But Mr Boshoff says this may not be easy, as they have resisted previous attempts to disarm them.
Arrest warrant
The rebel leader was detained in Rwanda after troops converged on his stronghold in the Congolese town of Bunagana.
"The ex-general Laurent Nkunda was arrested on Thursday 22 January at 2230 hours while he was fleeing on Rwandan territory after he had resisted our troops at Bunagana with three battalions," a Congolese-Rwandan official statement said.

Gen Nkunda has lost the support of some of his troops in recent weeks
Rebels with him were being urged to disarm, reports said.
Congolese Information Minister Lambert Mende Omalanga, told the BBC he welcomed the arrest.
"I think it is a good achievement for peace and security in this area and this region of Great Lakes," he said.
Mr Omalanga said he wanted Rwanda to extradite him to face justice in DR Congo.
DR Congo has issued an international warrant for Gen Nkunda's arrest following past accusations that his forces had committed atrocities.
Rwandan army spokesperson Major Jules Rutaremara told the BBC that General Nkunda was being held by the Rwandan forces in Rubavu district in western Rwanda, close to the border with the DR Congo.
But the Rwandan authorities have not yet issued any formal statement concerning his arrest.
Some of Gen Nkunda's forces - perhaps as many as 2,000 - are still said to be loyal to him.
The question now is whether they will fight, or whether they will join the new consensus and become integrated into the Congolese army, correspondents say.
The CNDP launched a major offensive in August 2008, which displaced more than a quarter of a million people in North Kivu and raised fears of both a humanitarian crisis and a wider regional war.
Correspondents say this may have been Gen Nkunda's undoing, by bringing huge international pressure on all sides to end the conflict in DR Congo.
Human rights group have accused CNDP forces, along with those of the government, of numerous killings, rapes and torture.
All sides in the Congolese conflict have also been accused of using the fighting as a pretext to loot eastern DR Congo's rich resources of minerals such as gold, tin and coltan, used in mobile phones.
Some five million people are estimated to have died as a result of almost 15 years of conflict in DR Congo, following the Rwandan genocide.
Source:BBC News

Tuesday, January 20, 2009

US PRESIDENT BARACK OBAMA!

Obama will soon be declared as a 44 US president, the history will write his name in the mind of young men and women of this day, old men and women of this day and school children of this day!

The dream of Martin Luther King is coming true this day!
To some of us inauguration of 44 US president, a black man,Obama, is speaking aloud one thing, that is "It doesn't matter you are born white or black, we all have equal rights to all opportunities around us"

Wishing him all the best!



Tuesday, December 2, 2008

TUWAKATAE VIONGOZI WACHAFU,WALAFI NA MAFISADI!!

Hakuna lisilowezekana katika sayari hii izungukayo!Kila jambo lina wakati wake, wakati hubadilika, binadamu hana budi kwenda na mabadiliko hayo vinginevyo atabaki nyuma na kuachwa na wakati.Kwa muda mrefu Afrika imefanywa kuwa nyuma kutokana na uongozi mbaya wa viongozi walafi wapenda madaraka, wenye utajiri wasioweza kuutolea maelezo, walioupata kutoka kwa kidogo kilichopaswa kuwafikia wananchi wao.

Kile kidogo ambacho kingeweza kuinua maisha ya wananchi wao wamekibinafsisha, ni mithili mfugaji mwenye kutamani kupata ongezeko la maziwa kwa ng'ombe wake bila ya kumuongezea lishe,kumtafutia majani mabichi, wametamani kukamua ng'ombe maziwa yote hata waone matone ya damu, na wametamani maziwa hata kwa ng'ombe dume!!!!

Afrika ambayo imepigania uhuru wake kuanzia miaka ya hamsini bado haijawa huru kiuchumi hata kifikra!!, wako wapi mashujaa wetu wa leo?

Wako wapi kina Julius Nyrere, Kwame Nkrumah, Samora Machel, Nelson Mandela wa leo?, ni lini walikoma kuzaliwa ndani ya Afrika viongozi mithili ya hao?, Bado tunashuhudia Afrika ikiliwa kwa nje na nchi tajiri na kwa ndani na viongozi walafi, hali ikiwepo kasi ndogo na sheria iliyolegezwa na nguvu ya pesa kuwazuia wailao kwa ndani pamoja na kukosa ujasiri wa kupambana na wale wailao kwa nje.

Mwalimu Nyerere wakati akizitetea nchi za dunia ya tatu, alipata kuwakemea mabepari, nchi tajiri,walipokuwa wakishinikiza tuwalipe madeni yao, hela waliiyotunyonya na kutukopesha, akawaambia ni sawa na kumtoa damu mgonjwa mahututi,Afrika iko mahututi kichumi bado!!, wazungu wale walimuelewa Mwalimu!!, Ni nani anayeendeleza mapambano hayo kwa kasi ile ile leo?

Leo tunaona jinsi siasa inavyokimbiliwa hata na wanataaluma, wanajua ni rahisi kuneemeka ukiwa huko,hasa kwa walio na dhamiri zilizokufa,wanaothubutu hata kuchota mapesa ya kununua madawa na kununua magari ya kifahari!!, wanasayansi wamekimbilia siasa, kwa staili hii maendeleo yakujaje?

Kuna ujasiri mwingi na thubutu kubwa ambayo viongozi wetu walio safi wanapaswa kutuonyesha, na wasipofanya hivyo, basi umma utawalazimisha kwani wakati wa mabadiliko ukifika hakuna awezaye kuuzuia, na atakayejaribu kufanya hivyo atakuwa anapambana na nguvu kubwa asiyoiweza!!

Hapa Tanzania tumeshuhudia mawaziri wawili Basil Mramba na Daniel Yona wakipandishwa kizimbani kujibu mashitaka ya jinsi walivyotuibia, tunahitaji mwendelezo wa mapambano haya dhidi ya wale wailao nchi nyetu kwa ndani kwani ni wengi na wasiopaswa kuongoza kwa wakati wa sasa!!

Tuwakatae kama Mwalimu alivyotuasa!!!

Tuko kwenye zama nyingine kabisa,, hakuna lisilowezeakana!!!!!